Home » Waziri Kuria Atangaza Ada Ya Lazima Kwa Biashara Zote Nchini

Waziri Kuria Atangaza Ada Ya Lazima Kwa Biashara Zote Nchini

Waziri wa Biashara Moses Kuria amethibitisha kwamba serikali ilikuwa ikifanyia kazi Sheria ya Baraza la Mawaziri la Kenya inayofanya kuwa lazima kwa kila biashara kusajiliwa kwa ada.

 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kongamano la tatu la Uwekezaji la Kimataifa la Kenya, Kuria amesema kuwa hatua hiyo ni kuhakikisha biashara na makampuni ya Kenya yanaingia katika mataifa mengine na pia kupata kutambuliwa kimataifa.

 

Katika taarifa yake, Waziri huyo amebainisha kuwa itakuwa ni lazima kwa wamiliki wa biashara kujiandikisha na mamlaka husika, akiongeza kuwa sheria hiyo itawasilishwa mbele ya Baraza la Mawaziri ndani ya siku 30.

 

Zaidi ya hayo, amesema kuwa baraza hilo litawaleta pamoja wafanyabiashara wanaolenga kuiweka Kenya kwenye ramani ya dunia katika masuala ya uwekezaji.

 

Kuria ameongeza kuwa hatua hiyo itafikia viwango vya kimataifa akiifananisha na Bunge la Marekani na Baraza la Uchina.

 

Amekariri kuwa itakuwa lazima kwa kila mfanyabiashara kujiandikisha kwa wahusika waku na kuongeza kuwa anafahamu kuwa wafanyabiashara wengine watapinga hatua hiyo.

 

Aidha Mawaziri 55 wa Biashara, wakiungana na Wakurugenzi Wakuu wa makampuni 100 bora barani Afrika, wameratibiwa kuhudhuria mkutano huo unaotarajiwa kuendelea hadi Mei 31 katika Hoteli ya Safari Park jijini Nairobi.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!