Home » Uhuru Awatimua Wanachama 10 Jubilee

Aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta amekabiliana vikali na wanachama walioasi alidai hawakuwa waaminifu kwa chama.

 

Akizungumza katika Uwanja wa Ngong Racecourse wakati wa Kongamano la Kitaifa la Wajumbe wa chama (NDC), Uhuru amebainisha kuwa wanachama hao walikiuka katiba ya chama kwa kuendeleza ajenda za vyama vingine vya kisiasa nje ya muungano wa Azimio la Umoja.

 

Kupitia kwa Katibu Mkuu wa Jubilee Jeremiah Kioni, kiongozi huyo amewatimua wanachama wafuatao kutoka nyadhifa zao mbalimbali:

 

Jimmy Angweny, Mbunge wa zamani wa Buuri Boniface Kinoti Gatobu, Naomi Shaban, Nelson Dzuya, Joshua Kutuny, Mutava Musyimi na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Kanini Kega.

 

Rachael Nyamaye, Advice Mundalo, Mkurugenzi Mtendaji Wambui Gichuru na Joel Kibe pia hawakusalia.

 

Aidha wanachama kumi wamechukua nafasi za wale waliotimuliwa.

 

Majina yaliyopendekezwa ya Chama cha Jubilee ni pamoja na;

 

Naibu kiongozi wa mkakati: Beatrice Gambo

Operesheni za naibu kiongozi wa chama: Maoka Maore

Naibu kiongozi wa chama wa mipango Joseph Manje

Naibu kiongozi wa chama – Kados Muiruri

Mwenyekiti- Saitoti Torome (PS)

Naibu katibu mkuu – Yasir Noor

Naibu Katibu Mwenezi – Pauline Njoroge

Mkurugenzi wa Kitaifa wa Uchaguzi – Jamleck Kamau

Mwenyekiti wa Wanawake Taifa – Maison Leshomo

mwenyekiti wa Taifa vijana, – Agnes Thumbi

Mratibu wa huduma za Vijana – Anthony Manyara

Baraza la Biashara – Nderitu Mureithi

Katibu wa Bunge – Amina Siyad

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!