Home » Wakenya Wajiuliza Maswali Jinsi Mdhibiti wa Bajeti Alikataa Maombi Ya Fedha Ya Kaunti 28

Wakenya Wajiuliza Maswali Jinsi Mdhibiti wa Bajeti Alikataa Maombi Ya Fedha Ya Kaunti 28

Kaunti 28 zimenyimwa nyongeza ya Shilingi bilioni 3.2 pesa taslimu na Mdhibiti wa Bajeti (CoB) katika muda wa miezi saba hadi Februari hasa kwa kukosa kuhalalisha ni kwa nini walihitaji fedha hizo.

 

Ripoti ya mdhibiti wa bajeti Margaret Nyakang’o inaonyesha zaidi kwamba ubadhirifu wa fedha ,bili zisizojulikana na mishahara ya juu ya nje ya kiwango cha kisheria ulisababisha kunyimwa pesa kwa vitengo vilivyogatuliwa.

 

Kaunti zilizoathirika na hali hiyo ni Narok, Nairobi, Nakuru na Kisii, ambazo zilinyimwa zaidi ya Shilingi milioni 200 kila moja, huku Narok ikiongoza kwa madeni mengi ya pesa, jumla ya Shilingi milioni mia 910.4.

 

Ripoti ya kuidhinishwa kwa matakwa inasema baadhi ya sababu zilizofanya Serikali ya Kaunti ya Narok kunyimwa pesa hizo ni ukosefu wa mpango kazi wazi wa kutekeleza miradi na kuzuiliwa kwa taarifa za ushuru kwa baadhi ya wasambazaji bidhaa kwa kaunti.

 

Kaunti ya Nairobi, ambayo ilikataliwa Shilingi milioni mia 525, maombi yake 10 yalikataliwa, tisa kati ya hayo yakiwa na mtendaji mkuu wa kaunti.

 

Ofisi hiyo pia ilikanusha ombi la kaunti la Shilingi milioni 6.9 milioni mnamo Desemba 9, iliyodaiwa kugharamia wakati wa kuapishwa kwa Gavana Johnson Sakaja.

 

Maombi mengine kadhaa yalikataliwa kuhusiana na madai ya kulipa malimbikizo na bili zinazosubiri ambazo kaunti haikuweza kuunga mkono.

 

Kaunti ya Nakuru pia haikuweza kupata zaidi ya Shilingi milioni 450, huku msingi wa kukataa ombi la Shilingi milioni 215 mnamo Januari 23 ukiwa uainishaji mbaya wa “Lapfund” inayosubiri bili kama matumizi ya maendeleo na Shilingi milioni 170 ikiwa madai ya ulipaji wa magari ambayo hayakuungwa mkono na maelezo ya ununuzi pamoja uthibitisho wa umiliki.

 

Usimamizi wa bajeti umesema katika kipindi cha miezi saba, ulipokea maombi ya kupokea fedha kwa kaunti mbalimbali takriban Shilingi bilioni 182.7, ambapo Shilingi bilioni 179.5 ziliidhinishwa.

 

Kaunti zilizoangazia matumizi ya kawaida chini ya bajeti ya maendeleo au ambazo uidhinishaji wa bajeti ulipingwa na mabunge na washikadau wengine kuhusu mchakato wa kuidhinisha bajeti hiyo pia zilikataliwa maombi ya ufadhili.

 

Kaunti Nyingine zilizorekodi maombi makubwa yaliyokataliwa ni Bungoma, Kisii, Kitui, Machakos, Turkana, Samburu na Machakos, kila moja zaidi ya Shilingi milioni 150.

 

Maombi 17 ya Kaunti ya Bungoma yalikataliwa, huku masuala yaliyoibuliwa na usimamizi wa bajeti yakiwa matumizi na vielezo visivyo sahihi kushindwa kwa wafanyakazi wa bodi kwenye mfumo wa IPPD kukosa kuunga mkono maombi hayo.

 

Mdhibiti wa bajeti Nyakango ameshauri kaunti ziwasiliane na Hazina ya Kitaifa na Benki Kuu ya Kenya ili kuharakisha mchakato wa hazina na kuongeza ufanisi katika utoaji wa fedha na uwajibikaji huku ikipunguza mwingiliano wa watu.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!