Home » Ajali Ya Ndege Yashuhudiwa JKIA

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege vya Kenya (KAA) Hii leo Jumatano, Mei 31, imetangaza tukio la ajali lililohusisha ndege iliyopaa juu katika Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA).

 

Katika taarifa yake imeripotiwa kuwa shughuli za uokoaji zinaendelea katika uwanja huo wa ndege, huku mamlaka ikiwa bado haijabaini chanzo cha tukio hilo.

 

“Ndege iliyokuwa ikipaa Nairobi ilikumbana na tukio JKIA asubuhi ya leo. Shughuli za haraka za uokoaji zinaendelea, zikiongozwa na timu zetu za kukabiliana na dharura Tunafanya kazi kwa karibu na mamlaka huku tunatanguliza usalama wa wote wanaohusika,” iliongeza taarifa hiyo.

 

Mdadisi wa ndani katika uwanja huo wa ndege aliyezungumza na BILLY O’CLOCK pia amekataa kutoa habari zaidi, akisema kuwa KAA ilikuwa inaandaa taarifa ya kina.

 

“Tunatafuta kufahamu tukio hilo – hatuwezi kuthibitisha ikiwa bado ni ajali. Subiri kwa taarifa kamili,”.

 

Walioshuhudia walidai kuona moshi ukiifunika ndege hiyo katika eneo la JKIA.

 

KAA bado haijafichua ikiwa ndege hiyo ilikuwa ikitua au kupaa, na ikiwa abiria au mizigo ilikuwa ndani.

Hakuna majeruhi walioripotiwa.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!