Home » ‘Ukishindwa kubali umeshindwa,’Malala Amwambia Raila

Katibu Mkuu wa UDA Cleophas Malala amemtaka kiongozi wa Muungano wa Azimio la Umoja wa Kenya Raila Odinga kuacha kuandaa maandamano na kukubali kushindwa katika Uchaguzi wa Rais wa Agosti 9, 2022.

 

Akizungumza katika eneo bunge la Malava katika Kaunti ya Kakamega leo Jumamosi wakati wa ibada ya shukrani iliyofanyika katika Shule ya Msingi ya Silungai, Malala amebainisha kuwa Odinga sasa anang’ang’ania katika jaribio la kujilazimisha kuingia katika serikali ya Kenya Kwanza.

 

Huku akirejelea jinsi alivyokubali kushindwa katika kinyang’anyiro cha ugavana wa Kakamega Agosti 2022 dhidi ya mshindi gavana Fernandes Barasa, Malala amemtaka Odinga kutulia nyumbani.

 

Kauli ya Malala inafanana na yale ya wanasiasa wengine wa Kenya Kwanza ambao katika wiki za hivi majuzi wamedai kuwa Odinga anaongoza maandamano ya Azimio ya kila wiki ya Azimio kwa matumaini ya kusaini makubaliano ya kisiasa na Rais William Ruto.

 

Odinga amewaagiza wafuasi wake kujitokeza barabarani mara mbili kwa wiki, siku za Jumatatu na Alhamisi, wakilalamikia serikali ya Rais Ruto kwa gharama ya juu ya maisha inayoshuhudiwa kote nchini.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!