Home » Mke Wa Samidoh Edday Asherehekea Siku Ya Kuzaliwa Kwa Binti Yao

Mke Wa Samidoh Edday Asherehekea Siku Ya Kuzaliwa Kwa Binti Yao

Edday Nderitu amesherehekea siku ya kwanza ya kuzaliwa kwa bintiye.

 

Binti ya mwimbaji wa Mugiithi, Samidoh, Neriah, alizaliwa mwaka wa 2022 wiki chache baada ya bintiye Karen Nyamu kuzaliwa.

 

Ili kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, Edday alimtaja bintiye kama baraka kwa familia yao Kisha akamtakia heri ya mwaka ujao.

 

Aliendelea kusema kwamba binti yake alikuja maishani mwake wakati alipomhitaji zaidi.

 

“Midomo ya waridi, macho yenye kung’aa na nywele nzuri hukufanya kuwa binti wa kifalme, umependeza maisha yetu kwa mwaka mzima sasa, ulikuja maishani mwangu wakati nilikuhitaji sana, wewe ni baraka kwa familia yetu, ukue katika hekima na busara. … Mungu akulinde na mabaya yote, HAPPY 1st BIRTHDAY BABY NERIAH #hakuna ila maombi @nimu_muchoki

 

Edday na Samidoh wana watoto wengine wawili pamoja, wa kiume na wa kike.

 

Miezi michache iliyopita, mtoto wa kwanza wa Samidoh na mkewe Edday Nderitu alifuzu masomo ya shule ya msingi.

 

Mama huyo wa watoto watatu alishiriki picha zake akiwa amevalia gauni na kofia ya kuhitimu, akimchangamsha kwa upendo.

 

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 12 yuko katika shule ya bweni.

 

“Ndoto zako ziwe kubwa kuliko hofu zako, matendo yako yawe na sauti kubwa kuliko maneno yako, na imani yako iwe na nguvu kuliko hisia zako,” Edday alinukuu.

 

Akizungumzia chapisho la mke wake, Samidoh alimsifu binti yake kwa mafanikio hayo.

 

Alisema kuwa amekuwa na changamoto kwani binti yake alihitimu kabla ya yeye.

 

“Haka kamegraduate mbele yangu aki. Inabidi nivue soksi sasa. Hongera sana mama mdogo.”

 

Samidoh alikutana na mkewe alipokuwa bado shule ya upili baada ya mkewe kuhamishiwa shule aliyokuwa nayo na muelewano baina ukashika kasi.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!