Home » Safari Ya Arsenal Europa Yafikia Ukingoni

Safari Ya Arsenal Europa Yafikia Ukingoni

photo courtesy

Goncalves aliifunga sporting lisbon bao la kusawazisha na kusaidia timu hiyo ya Ureno  kuwaondoa Arsenal kwenye Ligi ya Europa kwa ushindi wa penalti 5-3 katika mkondo wa 16 bora, Alhamisi usiku

 

 

Granit Xhaka alikuwa amewapa vinara wa Ligi ya Premia Arsenal uongozi katika kipindi cha kwanza katika mechi hiyo iliyochezwa  Uwanja wa Emirates.

 

Gonclave, kiungo wa kati wa Ureno alilazimisha muda wa ziada alipomlemea kipa wa Arsenal Aaron Ramsdale kwa mkwaju wa ajabu kutoka yadi 46 nje.

 

 

Ilikuwa ni Sporting ambao waliibuka na ushindi wa kushtukiza huku penalti  ya Gabriel Martinelli zikiokolewa na Antonio Adan kisha  Nuno Santos kupeleka mkwaju wa ushindi.

 

“Pigo kubwa ni dhahiri. Kulikuwa na nyakati katika dakika 75 za kwanza ambapo hatukuwa katika kiwango chetu. Tulitoa kila mpira na hatukuwa na uwezo wa kuchukua mchezo. Tulikuwa na nafasi kubwa kumaliza mchezo. Lazima tujiangalie na kwa nini hatukuwa wazuri vya kutosha kupita.” Alisema Artetaa

 

Arsenal hawajashinda taji lolote la Uropa tangu wanyanyue Kombe la Washindi 1994 na kungoja kwao kutaendelea kwa mwaka mwingine.

 

Lakini The Gunners wangebadilisha kwa furaha mafanikio ya Ligi ya Europa kwa taji lililokuwa likisubiriwa kwa muda mrefu la Premier League.

 

Arsenal wapo mbele kwa pointi tano dhidi ya Manchester City walio katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England huku wakisaka ubingwa wa kwanza tangu 2004.

 

“Tumebakisha michezo 11. Mchezo wetu unaofuata na Palace ni fainali. Kazi yote tunayofanya sasa hivi lazima iwe kuelekea Palace. Tunapaswa kuwa bora zaidi ya mchezo huu,” Arteta alisema.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!