Majizo Amvika Lulu Maua Yake
Siku ya wanawake duniani watu wengi wameweza kuonesha hisia zao za mapenzi juu ya wanawake ambao kwao wamekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo yao.
Moja kati ya watu hao ni mkurugenzi wa kituo cha habari cha E media ambaye ni maarufu kwa jina la Majizzo baada ya kumtaka mke wake kipenzi Elizabeth Michael kama mwanamke wake wa nguvu.
Katika ukurasa wa Instagram wa Majizo alithibitisha Hilo mara baada ya kuandika juu ya umuhimu wa mkewe wake huyo na kuwa Elizabeth Michael (Lulu) kuwa ndiye mwanamke wake wa nguvu.
Mwanamke ni nani kwangu?
Ni mama aliyepata taabu tumboni mwake na baadaye mikono yake ikatulea kwa taabu sana. Unapomzungumzia mwanamke kwangu mimi unazungumzia Elizabeth Michael…..
Majizzo na Elizabeth Michael ni wanandoa ambao wameoana kwa miaka zaidi ya miwili iliyopita huku wakibarikiwa kuwa na watoto wawili wakiwa ndani ya ndoa yao hiyo