Home » Jimal Roho Safi Akanusha Kumdhulumu Amira

Baada ya mfanyabiashara maarufu Jimal Roho Safi kushutumiwa na mke wake wa zamani kwa unyanyasaji, ameamua kutoa majibu yake kwa tuhuma hizo kuu.

 

Kulingana na Amira, mwanabiashara huyo alikuwa mnyanyasaji na alimshambulia kimwili walipokuwa kwenye ndoa.

 

Amira alitumia Instagram yake na kumshutumu Jamal kwa kumnyanyasa kimwili alipokuwa na ujauzito wa mtoto wao wa tatu, na kusababisha mimba kuharibika.

 

Baba wa watoto wawili, ambaye amegonga vichwa habari hivi majuzi akidai kuwa single ni kitu kizuri, alikanusha shutuma hizo, na kuongeza kuwa Amira alikuwa akitafuta tu kuhurumiwa na mitandao ya kijamii.

 

“Amira ni mwongo, kama angekuwa mjamzito, angesambaza habari hizo kwa ulimwengu mzima. Sote tulikubaliana kupata watoto wawili kwa vile anaumwa mgongo. Hakuna wakati tuliamua kupata mtoto mwingine.”

 

Kulingana na Jimal, daktari alimshauri Amira dhidi ya kupata ujauzito tena na pia akamwambia apunguze uzani kutokana na hali yake ya kiafya.

 

Jimal tayari ameendelea na Wangari Thiong’o na kwa pamoja, wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!