Home » Kanisa La CITAM Lahoji Mahakama Kuu Kuhusu Haki Ya LGBTQ

Baadhi ya viongozi wa makanisa wameikosoa Mahakama ya Juu ya Kenya kuhusu uamuzi wake kuhusu jumuiya ya LGBTQ.

 

Katika taarifa ya Christ is the Answer Ministries (CITAM) ambalo ni mojawapo ya makanisa makubwa nchini Kenya yenye matawi 15 kote nchini limesema kuwa uamuzi huo unakinzana na sheria zilizopo kwa sasa.

 

Alipokuwa akinukuu maandiko, Askofu Calisto Odede hata hivyo amesisitiza kwamba ushoga ni kinyume na mafundisho ya Biblia na kanuni za kitamaduni barani Afrika.

 

Amewataka wakenya kudumisha uadilifu kwa kupinga majaribio yoyote yanayolenga kumomonyoa kanuni na maadili yanayoheshimiwa ya jamii.

 

Mahakama ya Juu ya Kenya mnamo Ijumaa iliamua kwamba uamuzi wa Bodi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kuwazuia wapenzi wa jinsia moja kuunda vikundi vinavyotambulika ni wa kibaguzi.

 

Kanisa hilo limesema kuwa licha ya ushoga kuwa haramu nchini Kenya, wanachama wa wasagaji, mashoga, watu wa jinsia mbili, waliobadili jinsia, watu wanaohojiwa (LGBTQ) bado wana haki ya kujumuika.

 

Maoni kama hayo yameungwa mkono na Kanisa la Redeemed Gospel Church of Kenya.

 

Askofu Mkuu Arthur Kitonga amesema makundi hayo hayafai hata kuruhusiwa nchini Kenya, taifa ambalo linashikilia sana mafundisho ya Kikristo.

 

Akizungumza katika Kijiji cha Kaloleni, Kaunti ya Machakos, Kitonga amesema kuwa kuruhusu mambo hayo kunaweza kuleta laana nchini, kwani ni sawa na kuvunja sheria za Mungu.

 

Mchungaji Joseph Ngutu wa Kanisa la Redeemed Gospel Church Tala kwa upande wake amesema kuwa mahakama inapaswa kuhakikisha maamuzi yanaenda sambamba na mafundisho ya Biblia.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!