Home » Mbunge Nimrod Mbai Amdhulumu Afisa Wa Kenya Power

Mbunge Nimrod Mbai Amdhulumu Afisa Wa Kenya Power

Mbunge wa Kitui Mashariki Nimrod Mbai ameangaziwa katika mitandao ya kijamii kwa kumfanyia fujo mhandisi wa Kenya Power ambaye aliripotiwa kutaka kukata laini ya umeme katika nyumba ya mbunge huyo eneo la Kitengela, Kaunti ya Kajiado.

 

Katika video ambayo sasa inasambaa kwenye mitandao ya kijamii, mbunge huyo anaonekana akiwarushia matusi maafisa wa Kenya Power kabla ya kumpiga kofi mmoja wao wakati wa kisa hicho kilichotokea.

 

Mbai vile vile alinyoosha mkono na kujaribu kuchomoa bastola yake wakati wa kisa hicho.

 

Maafisa hao wa KPLC hata hivyo walifanikiwa kukata njia ya umeme siku ya Jumanne baada ya kufika katika majengo hayo pamoja na polisi.
Maafisa hao waliovalia pia waliwakamata wafanyikazi wawili walioajiriwa katika jumba la kifahari ambalo linajengwa kwa sasa.

 

Inasemekana maafisa hao wa kampuni ya umeme walipata mita ya umeme na nyaya za ziada kutoka kwa Mamlaka ya Usambazaji Umeme Vijijini nyumbani kwa mbunge huyo.

 

 

Maafisa hao wa Kenya Power wanadai kuwa mbunge huyo alikuwa ameweka njia haramu ya umeme katika majengo hayo yenye urefu wa zaidi ya kilomita moja.

 

Afisa mkuu wa usalama wa KPLC aliambia billy o’clock kwamba njia hiyo ya umeme haramu ni hatari kwa kuwa ilikuwa inapakia transfoma ya umeme iliyo karibu.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!