Home » Stanley Omondi Apuuzilia Mbali Kuhusu Kuachana Na Crazy Kennar

Stanley Omondi Apuuzilia Mbali Kuhusu Kuachana Na Crazy Kennar

Content Creator nchini Kenya Stanley Omondi amepuuzilia mbali uvumi kwamba alikosana na mcheshi wa mtandaoni Crazy Kennar.

 

Akizungumza kwenye Instagram, Stanley Omondi amesema yeye ni mwigizaji wa sinema na pia mburudishaji na anafanya vizuri nyuma ya kamera na kwa timu iyo hiyo ya Kennar.

 

Stanley Omondi amesema alikuwa na mazungumzo na Crazy Kennar na ingawa haikuwa rahisi, alilazimika kufanya hivyo kwa sababu alihitaji kukuza Brand yake.

 

Muigizaji huyo amesema uvumi umekuwa ukienea kwenye mitandao ya kijamii kuwa Kennar aliwaondoa wanaume wawili kwenye timu yake na kuamua kufanya kazi na wanawake pekee.

 

Ameongeza kuwa hakuna kitu kibaya kati yao na hivi karibuni kutakuwa na video ambapo atatangazwa kuwa mkurugenzi wa upigaji picha.

 

“Tafadhali acheni kueneza propaganda, kama nyie watu mnapenda ninachofanya, sapotini na endeleeni kusukuma yaliyomo lakini msijaribu kumuangusha Crazy Kennar. Huyu jamaa amekuwepo kwa ajili yangu na nitaendelea kuwa naye. bado ninafanya kile nilichokuwa nikifanya, ukweli kwamba huwezi kuniona kwenye skrini kwa Kennar haimaanishi kuwa aliniacha na kuwa upande wa wanawake pekee.”

 

Omondi pia alimsifu Crazy Kennar kama Content Creator bora na akawataka mashabiki kuendelea kumuunga mkono.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!