Home » Mbunge Wamumbi, Betty Maina Waanzisha Sherehe Za Kitamaduni Za Ndoa

Mbunge Wamumbi, Betty Maina Waanzisha Sherehe Za Kitamaduni Za Ndoa

Mbunge wa Eneo Bunge la Mathira Eric Wamumbi alianza raundi ya kwanza ya mazungumzo ya mahari ya kimila ya Kikuyu Jumamosi, kwa ajili ya kumuoa Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Murang’a Betty Maina.

 

Mbunge huyo aliomba usaidizi wa marafiki na familia yake, wakiwemo wabunge Ndindi Nyoro, Babu Owino, Anne Waiguru, Mutahi Kahiga, Sylvanus Osoro, na Gathoni Wamuchomba, kwa ajili ya ‘Kuhanda Ithigi,’ hafla ambayo bwana harusi huwafahamisha wakwe zake kuhusu nia yake kuoa.

 

Huku ‘Kuhanda Ithigi’ ikikamilika ,mbunge huyo atatarajiwa kufanya safari nyingine muhimu kwa wakwe zake, wakati huu kwa ajili ya ruracio- sherehe halisi ya kulipa mahari.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!