Home » Mwanamke Wa Waume Watatu Asema Anawaridhisha Wote

Mwanamke mmoja kutoka Nigeria amewaacha wengi wakiwa na mshangao baada ya kusimulia kisa cha uhusiano wake na wanaume watatu kwa wakati mmoja.

 

Nellie ni mama wa watoto wawili na ana waume watatu, Jimmy, Danny na Hassan ambao wote wamekuwa marafiki wakubwa kwa muda mrefu.

 

Mwanamke huyo na waume wake watatu wanaishi katika nyumba moja na wanaume huona fahari kuwa na mke wao popote waendapo.

 

Katika mahojiano na Afrimax, Nellie alisema ameishi na waume zake watatu kwa miaka mitatu. Aliwahi kuolewa na mume kwa miaka minane lakini alifariki kwa ajali ya gari akiwaacha watoto wake wawili.

 

Baada ya kufiwa na mume wake, aliendelea kuishi na kaka yake katika nyumba moja na muda mfupi baadaye wakawa mke na mume.

 

Alikutana na mume wake mwingine kwa namna tofauti. Alikuwa amemaliza shule na alikuwa hana kazi. Nellie alimwonyesha upendo, akampeleka nyumbani na akawa mume wake.

 

Mume wake mwingine alikuwa mpweke alipokutana naye. Alikuwa amevunjika moyo na alihitaji mtu wa kumwambia maneno mazuri.

 

Wawili hao walishiriki mazungumzo ya kina, wakawa marafiki. Alikubali ukweli kwamba alikuwa na mume mwingine na akahamia kwake.

 

Nellie ni mfanyabiashara wa magari na waume wake hawana kazi. Yeye huwapa mahitaji na hata amewanunulia magari wote.

 

Wa mume wana vyumba vyao na Nellie ana chumba chake. Wanaheshimiana na wote wanaishi kwa amani.

 

Linapokuja suala la kujamiana, wanapanga ratiba chumbani naye kwa zamu.

 

Nellie anasema waume  humridhisha na wote wamejifunza kuwa na furaha na kushiriki kila kitu.

 

Nellie anasema kuishi na waume watatu kunamfurahisha na anaamini wana furaha na kuridhika na hawawezi kumsaliti.

 

Anajitahidi sana kuhakikisha wanaume wake hawakosi chochote.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!