Home » TSC Yafichua Kaunti Zinazopendwa Zaidi Na Walimu

Kaunti ya Nairobi ndiyo eneo linalopendelewa zaidi na walimu wanaotafuta uhamisho kufuatia hatua ya serikali kutekeleza sera za walimu, kulingana na data rasmi kutoka kwa Tume ya Kuajiri Walimu (TSC).

 

Walimu elfu 36,277 Kitaifa waliomba uhamisho kati ya Novemba 1 mwaka jana na Januari 31 mwaka huu, kulingana na data iliyowasilishwa na tume hiyo ya TSC kwa Kamati ya Seneti kuhusu Elimu.

 

Kati ya maombi hayo ya uhamisho, elfu 14,733 yalioanishwa na kuidhinishwa huku elfu 21,544 yakisubiri.

 

Katika kipindi hicho, walimu elfu 1,885 waliomba kuhamishwa hadi jiji kuu dhidi ya 76 walioomba kuhamishwa kutoka Nairobi.

 

Hata hivyo, ni maombi 41 tu kati ya elfu 1,162 kwa shule za msingi na manne kwa shule za sekondari kati ya mia 723 yalikuwa yameidhinishwa kufikia mwisho wa Januari.

 

Makubaliano ya kubadilisha sera ya ugatuzi yamo katika kanuni za makubaliano ya makubaliano ya pamoja yasiyo ya kifedha (CBA) ya walimu yaliyotiwa saini na TSC.

 

Aidha, itakumbukwa kwamba Suala hilo pia lilikuwa mada ya kampeni huku Muungano wa Kenya Kwanza ukiahidi kulifuta mara watakapochukua mamlaka.

 

Kaunti ya Kajiado pia iliibuka kuwa mojawapo ya kaunti zinazopendelewa zaidi baada ya kupokea maombi mia 237 ya uhamisho wa walimu katika shule za upili dhidi ya 94 walioomba kuhamishwa kutoka kaunti hiyo.

 

Kwa walimu wa shule za msingi, mia 486 waliomba kufanya kazi katika kaunti dhidi ya mia 434 walioomba kupelekwa kwingine.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!