Home » Crystal Palace Imemfuta Kazi Kocha Mkuu Patrick Vieira

Crystal Palace Imemfuta Kazi Kocha Mkuu Patrick Vieira

Crystal Palace imetangaza kumfukuza kazi kocha mkuu Patrick Vieira siku ya Ijumaa asubuhi. The Eagles hawajapata ushindi wowote tangu mwanzoni mwa mwaka huu, na kujikuta wakishuka daraja ghafla.

 

 

Licha ya kuwa katika nafasi ya 12, wako juu ya wanaoshikilia nambari18 na alamu 3 pekee.

 

 

Ni msururu huo mbaya  ambayo imechangia Patrick  Vieira kupoteza wadhifa wake baada ya takriban miaka miwili kwenye usukani, huku harakati za kumtafuta bosi mpya zikiendelea.

 

 

Mwenyekiti Steve Parish alisema katika taarifa yake kwenye tovuti ya klabu kuwa wamesikitishwa sana na matokeo mbaya ambayo imechangia uamuzi huo wa kumpiga kalamu mfaransa huyo.

 

 

“Ni kwa masikitiko makubwa kwamba uamuzi huu mgumu umefanywa. Hatimaye, matokeo ya miezi ya hivi karibuni yametuweka katika hali mbaya ya ligi na tuliona mabadiliko ni muhimu kutupatia nafasi bora zaidi ya kuhifadhi hadhi ya Ligi Kuu. Hiyo ilisema, athari ya Patrick tangu ajiunge nasi msimu wa joto wa 2021 imekuwa kubwa, na anazingatiwa sana na mimi, na wenzake wote. Aliiongoza timu hadi nusu fainali ya Kombe la FA Wembley na ya 12 ya heshima. Walimaliza msimu uliopita wakicheza kandanda ya kusisimua, ambayo ilikuwa kampeni yenye changamoto na muhimu kwa klabu kutokana na mabadiliko tuliyofanya kwenye kikosi kabla ya kuwasili kwake,” kasema Parish.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!