Home » Rais William Ruto Atangaza Uchimbaji Upya Wa Mabwawa Ya Arror Na Kimwarer

Rais William Ruto Atangaza Uchimbaji Upya Wa Mabwawa Ya Arror Na Kimwarer

Rais william Ruto ametangaza  kuanzishwa upya kwa uchimbaji wa mabwawa ya Arror na  Kimwarer katika kaunti ya Elgeyo Marakwet na lile la Itare maeneo ya Kuresoi,  kaunti ya Nakuru

 

 

Rais alitangaza hayo baada ya kukutana na kufanya  kikao na rais wa Italia bwana  Sergio Mattarella  ambaye yuko nchini Kenya kwa ziara ya siku tatu ya kikazi.

 

 

Mabwawa haya matatu yalizua utata mkali wa  ufisadi na kisiasa katika serikali ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta na  kupelekea aliyekuwa waziri  Henry Rotich kufunguliwa mashtaka kortini.

 

 

Hata hivyo, Ruto amesema mikakati kabambe imewekwa  ya kuyachimba mabwawa ya Arror, kimwarer na itare baada ya makubaliano mapya kuafikiwa

 

 

Rais mastaafu Uhuru Kenyatta mwaka wa 2019 alifutitia mbali kandarasi ya uchimbaji bwawa hizo baada ya kubainika pesa zilifujwa katika mradi huo.

 

 

Ruto pia ametangaza serikali ya Kenya na Italia imeafikiana kuondoa kesi iliyokuwa mahakamani ya kufutitia mbali kandarasi hiyo na badala yake viongozi hao wamekubaliana kujengwa mabwawa ya kisasa  litakalogharimu bilioni 66.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!