Home » Mwanaume ,23, Afariki Baada Ya Kudaiwa Kuruka Kutoka Orofa Ya Sita Kasarani.

Mwanaume ,23, Afariki Baada Ya Kudaiwa Kuruka Kutoka Orofa Ya Sita Kasarani.

Familia moja inapitia hali ya majonzi baada ya jamaa yao kupatikana amefariki baada ya kudaiwa kuruka kutoka orofa ya sita huko Kasarani.
Blair Muthomi amekumbana na kifo chake wiki chache tu baada ya kuhitimu katika chuo kikuu.

 

Alikuwa mwanafunzi wa uhandisi wa mitambo katika Taasisi ya Mafunzo ya Kiufundi ya Nairobi. Marehemu aliishi na vijana wengine wawili wakisaidiana kuchangia pesa za kodi.

 

 

Wenzake waligundua mwili wake muda mfupi baada ya kuanguka na kuwaarifu polisi.

 

Msimamizi katika eneo la ujenzi lililo karibu na aliyetambuliwa kama Macharia alikuwa akifungua lango ili wafanyikazi kuhamisha vifaa kwenye paa la jumba hilo wakati mwenzie Muthomi alipomfuata.

 

 

Marafiki zake Muthomi Wawili hao wamekamatwa kama watu wanaohusika na vile vile kutoa taarifa zaidi.

 

Kulingana na wataalamu wa magonjwa, Muthomi alifariki kutokana na majeraha ya tumbo na kifua ambayo yameendana na kuanguka.
Familia iliyofadhaika imewataka maafisa wa upelelezi kuchunguza suala hilo na kuhakikisha haki inatendeka.

 

Kifo cha Muthomi kilitokea mita chache kutoka ambapo Jeff Mwathi mwenye umri wa miaka 23 alikumbana na kifo chake cha ghafla.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!