Home » Wachimba Migodi Wavamiwa Nairobi

Watu watatu waliuawa na wengine watatu kujeruhiwa jana Jumatatu baada ya kushambuliwa na wachimba migodi haramu katika kichimbo cha migodi cha Karebe karibu na Kibigori, Kaunti ya Nandi.

Kulingana na taarifa kutoka kwa Karebe Gold Mining Limited ilionyesha kuwa marehemu walikuwa wakifanya kazi katika eneo hilo wakati shambulio hilo lilipotokea mwendo wa saa 4.00 alasiri.

Kampuni hiyo ilidai kuwa mabishano na mgodi pinzani yangeweza kusababisha shambulio hilo ikishutumu mamlaka husika kwa ulegevu wa kukomesha shughuli za uchimbaji madini ndani ya eneo linalozozaniwa.

Kampuni ya Karebe ina leseni ya kufanya kazi nchini Kenya, na imekuwa ikifanya kazi katika eneo la Chemase katika wadi ya Chemilil kwa miaka 13 iliyopita.

Kampuni hiyo hata hivyo imekumbwa na misukosuko katika miaka michache iliyopita kutokana na mzozo wa ardhi kati ya Karebe na Kampuni ya uchimbaji madini ya Nandi/Chemase huku eneo la kuvutia likiwa Nandi Escarpment ambalo lina hazina kubwa ya dhahabu.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!