Home » Wakenya Wahimizwa Kutotumia Vifaa Vya DNA Vinavyozungumziwa Nchini

Wakenya Wahimizwa Kutotumia Vifaa Vya DNA Vinavyozungumziwa Nchini

Wizara ya Afya, kupitia Bodi ya Dawa na Sumu(PPB), imeonya Wakenya dhidi ya 
kutumia vifaa vinavyozungumziwa sana nchini vya kupima  DNA nyumbani 
kwani vifaa hivyo havijaidhinishwa.
Haya yanajiri baada ya habari kuenea sana Kenya kwamba Wakenya sasa 
wanaweza kukusanya chembechembe zao za DNA kwa uchunguzi wa nyumbani, huku 
vifaa hivyo vikisemekana vinapatikana katika maduka mbali mbali ya dawa kwa 
bei ya reja reja ya takriban Ksh.800.
Katika taarifa yake kwa vyumba vya habari hii leo,PPB imesema haijatoa mwanga
wa uuzaji wa vifaa hivyo vya majaribio, na kuwashauri Wakenya kuwa macho 
na wauzaji wa rejareja hao.
Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa bodi hiyo Dkt. Fred Siyoi katika taarifa hiyo
amewataka Wateja kuripoti kwa PPB iwapo watakutana na muuzaji yeyote 
anayeuza bidhaa zinazohusiana.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!