Waziri Malonza Aweka Historia Baada Ya Kuchaguliwa Kuongoza Nchi 6

Kenya imepata mafanikio makubwa baada ya Katibu wa Baraza la Mawaziri la Utalii, Peninah Malonza kuweka historia kwa kuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kuwa Rais wa Baraza la Utawala la Kikosi Kazi cha Makubaliano ya Lusaka (LATF).
Uchaguzi wake uliidhinishwa wakati wa mkutano wa ngazi ya juu uliofanyika na nchi sita wanachama mnamo jana Alhamisi, Juni 29.
Katibu wa Baraza la Mawaziri la Utalii atasimamia shughuli za nchi wanachama kwenye Mkataba wa Lusaka, ambazo ni Kongo (Brazzaville), Kenya, Lesotho, Liberia, Tanzania na Zambia.
Pia atawasiliana na Ethiopia, Afrika Kusini na Eswatini, ambao wametia saini mkataba huo.
Malonza pia aliapa kutumia fursa hiyo kutetea uharakati wa hali ya hewa ambao alibainisha kuwa utasaidia nchi wanachama kukabiliana na janga la wanyamapori.
Mbali na harakati za tabianchi, Malonza alizitaka nchi wanachama kuanzisha mageuzi mapya ya kukamata na kuacha ujangili, jambo ambalo alilalamikia kutishia kuwepo kwa mimea na wanyama porini.
Naibu Gavana huyo wa zamani wa Kitui alizisihi zaidi nchi wanachama kuongeza rasilimali ili kusaidia kukabiliana na changamoto za wanyamapori.
Waziri wa Utalii wa Kenya alichukua nafasi kutoka kwa Rodney Sikumba, Waziri wa Utalii wa Jamhuri ya Zambia.
Kabla ya kuchaguliwa, Malonza aliwahi kuwa Makamu wa Rais wa Baraza la Utawala la Mkataba wa Lusaka.
Mwanasheria Mkuu Justin Muturi alikaribisha maazimio hayo mapya akiongeza kuwa yalikuwa muhimu katika kuongeza mafanikio yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa Mkataba wa Lusaka.