Home » Cleophas Malala Afichua Viongozi Wa Azimio Wanaotaka Kujiunga Na Ruto

Cleophas Malala Afichua Viongozi Wa Azimio Wanaotaka Kujiunga Na Ruto

Katibu wa United Democratic Alliance Cleophas Malala amewakashifu wanasiasa wa Azimio akiwaita wanafiki wanaojifanya watetezi wa umma huku wakifuata masilahi ya kibinafsi.

 

Akizungumza wakati wa mazishi wa aliyekuwa mwanasiasa, Joseph Hamisi, Malala alimsuta Naibu Gavana wa Kakamega Ayub Savula akidai kuwa alimpigia simu akiomba kujiunga na serikali katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2027.

 

 

Alihoji ni kwa nini wanasiasa wa Azimio hawakabiliani na Rais William Ruto wanapozuru Ikulu.

 

“Ukweli wa mambo ni kwamba mkienda Ikulu, ninyi nyote hamkabiliani na William Ruto kuhusu suala hili. Mambo haya mnasema tu kwenye mikusanyiko na mazishi.

“Jana (Ijumaa) nilikuwa na Rais, Ayub Savula alinipigia simu na kuniomba niingie serikalini katika uchaguzi ujao, hamjataja chochote kuhusu kodi, mkimdhalilisha rais na sisi tutafanya hivyo hivyo nimekutaja kwa majina,” Malala alifoka.

 

Zaidi ya hayo, alipuuzilia mbali kujiuzulu kwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Seth Panyako kutokana na utata wa mfuko wa nyumba. Akizungumzia hilo, Malala aliorodhesha uongozi wa UDA na kuashiria kuwa Panyako hayupo uongozini

 

Viongozi Hao ni pamoja na Gavana Cecil Mbarire (Mwenyekiti), Hassan Omar (Naibu Mwenyekiti), Malalah (Katibu Mkuu) na Japheth Nyakundi (Mweka Hazina).

 

“Huu ni uongozi wa UDA. Seth Panyako alijiuzulu bila chochote,” alisema.

 

Katibu Mkuu wa UDA pia aliwakashifu wanasiasa ambao walikosoa ushuru wa nyumba kwenye hafla za kijamii na sio kwenye vikao maalum kama vile Bunge ambapo wangeweza kuwasilisha maswala mbele ya Bunge.

 

“Asilimia 3 ya mchango wa nyumba sio suala la kukosolewa katika mazishi na mikusanyiko isiyo rasmi; Fanya hivyo Bungeni,” alisema.

 

Panyako, ambaye alitoa tangazo hilo katika hafla hiyo ya mazishi, alikuwa amedokeza kuwa sababu yake ilichochewa na nia yake ya kusimama na Wakenya.

 

Alishikilia kuwa hana chaguo ila kujiondoa katika chama tawala.

 

“Nimeamua kuambatana na Wakenya kwa sababu wakati wa kampeni tulikuwa tunasema kazi ni kazi, pesa mfukoni. Sasa wanasema, Kazi ni kazi, pesa kwa serikali,” alisema.

 

Akizungumzia hilo, alithibitisha kwamba alifanya uamuzi huo baada ya kujadili suala hilo na rais huku akishikilia msimamo wake wa kupinga hazina ya nyumba.

 

“Nilizungumza na Rais saa 7:00 siku na ilionekana nisingeweza kuendelea na jukumu langu kutokana na kupinga mfuko wa nyumba na gharama kubwa ya maisha.

 

“Kwa hiyo, kwa niaba ya rafiki yangu marehemu (Hamisi), nataka nitangaze kuwa nimejiuzulu nafasi yangu ya UDA,” alisema.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!