Home » Mudavadi Kufika Mbele Ya Bunge

Mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi atafika mbele ya Bunge la Kitaifa leo hii Jumatano kujibu maswali ya wanachama.

 

Mudavadi anatarajiwa kujibu maswali kuhusu hatua zinazochukuliwa ili kupunguza bei ya bidhaa muhimu na mafuta, na kukabiliana na kushuka kwa shilingi ya Kenya dhidi ya sarafu nyinginezo.

 

Tangazo hilo lilitolewa wiki jana na Kiongozi wa Wengi Kimani Ichung’wah, wakati wa taarifa katika Bunge la Kitaifa.

 

Katika kikao hicho kitakachofanyika kwa mujibu wa Kanuni ya Kudumu ya sheria kipengele cha 42-A (5) na (6), waziri mwenye mamlaka pia atashughulikia maswali yanayohusiana na utoaji na usambazaji wa chakula cha msaada katika maeneo yenye ukame na njaa kali, kama yalivyoulizwa na Mbunge wa Kamukunji Yusuf Hassan.

 

Muonekano huo unatarajiwa kutoa mwanga kuhusu juhudi za serikali kukabiliana na matatizo ya sasa ya kiuchumi yanayoikabili nchi.
Mawaziri; Kindiki Kithure wa usalama wa (Ndani), Kipchumba Murkomen wa (Barabara na Uchukuzi) na Soipan Tuya wa (Mazingira) tayari wamefika mbele ya bunge hilo.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!