Home » Harmonize Aweka Wazi Furaha Yake

Mwimbaji wa Bongo, Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize ana furaha tele baada ya makamu wa rais wa Marekani, Kamala Harris kuorodhesha wimbo wake ‘Single Again’ miongoni mwa nyimbo anazozipenda zaidi za wasanii wa Afrika.

 

Siku ya Jumatatu, Kamala Harris alitoa orodha rasmi ya kucheza ya muziki anaoupenda zaidi wa Kiafrika kwenye Spotify kama njia ya kutangaza ziara yake ya sasa ya bara, kulingana na jarida la Billboard.

 

“Orodha ya kucheza, yenye jina la ‘Safari Zangu: Ghana, Tanzania, na Zambia,’ inapatikana kwenye jukwaa ‘kukuza wasanii na sauti kutoka kwa safari zangu’ katika nchi hizo,” alielezea.

 

Wimbo wa Konde Boy ‘Single Again’ ulishika nafasi ya nane kwenye orodha ya nyimbo zinazopendwa na makamu wa rais wa Marekani.

 

Wakati akijibu, bosi wa Kondegang alimshukuru Harris kwa kuibua vipaji maalum kutoka bara la Afrika.

 

“Inafurahisha sana kwa Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris kutambua vipaji vya Afrika,” alisema kwenye Instagram.

 

Mwimbaji huyo wa Bongo aliendelea kung’ara kuhusu uhusiano mzuri kati ya Marekani na Tanzania huku akimkaribisha makamu wa rais katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

 

“Uhusiano kati ya Tanzania na Marekani ni moja ya fahari yetu. Tafadhali jisikie uko nyumbani unapokuja kutembelea. Ni heshima kubwa,” alisema.

 

Makamu wa rais wa Marekani aliwasili Ghana Jumapili, Machi 26, kwa safari yake ya kwanza barani Afrika ofisini, na atazuru Tanzania leo hii Jumatano na Zambia siku ya Ijumaa kabla ya kurejea Marekani Jumapili.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!