Home » MCA Tricky Apata Shinikizo La Kuoa

Mcheshi MCA Tricky yuko chini ya shinikizo la kuoa na kupata watoto mwaka huu.

 

Katika mahojiano na mwanablogu mmoja humu nchini, mcheshi huyo alisema mama yake hataki kusikia kitu kingine chochote mwaka 2023 ila kuoa licha ya kusema anachumbiana lakini bado hajamtambulisha kwa mama yake.

 

“Lazima niwe na uhakika kabla ya kumtambulisha kwa mama yangu,” alisema na kuongeza kuwa anapanga kutulia mwaka huu baada ya kutimiza miaka 30.

 

“Mama yangu ananikasirikia kwa sababu anadhani ninapaswa kuwa na watoto watatu.

 

“Sitafichua mengi kwa mashabiki wangu, hata baada ya kuweka mambo hadharani.”

 

Kwa upande mwingine MCA Tricky ametangaza onyesho lake lijalo, ‘A Tricky Comedy Circuit’, litakalofanyika Nairobi Cinema mnamo Machi 31.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!