Home » Gladys Shollei: Acha Uhuru Aandikie IG Barua kuhusu Usalama Wake

Gladys Shollei: Acha Uhuru Aandikie IG Barua kuhusu Usalama Wake

Naibu Spika wa Bunge la Kitaifa Gladys Boss Shollei amependekeza kuwa Rais mstaafu Uhuru Kenyatta aandikie barua Inspekta Jenerali wa polisi Japhet Koome ili kuuliza  kilichosababisha kupunguzwa kwa usalama wake.

 

Shollei, ambaye ni Mwakilishi wa Wanawake wa Uasin Gishu, amebainisha kuwa hatua ya Koome imechukuliwa visivyo na wanachama wa Azimio la umoja one-kenya ili kutoa hisia kwamba ilichochewa kisiasa.

 

Shollei amewashauri wanasiasa kujiepusha na kukashifu hatua ya inspekta jenerali Koome na badala yake wawasilishe hoja zao na ukweli kama ilivyotajwa kisheria.

 

Aidha, amesema kuwa mashambulizi, ambayo anadai yanasemwa katika mikutano ya kisiasa, yanazua ghasia zisizo na sababu kutoka kwa umma na si kila kitu kinafaa kuingizwa siasa.

Ikumbukwe siku moja baada ya walinzi wa usalama wa Uhuru kupunguzwa, inspekta jenerali Koome alifafanua kuwa Serikali haikumlazimisha kuidhinisha mabadiliko ya maafisa wa usalama wa maafisa waliostaafu wa serikali na kwamba anafanya kazi kwa mujibu wa masharti ya sheria.

 

Kwa mujibu wa Sheria, rais mstaafu anayo haki ya kuwa na walinzi wasiozidi sita kwa matumizi ya kitengo cha kibinafsi na cha kusindikiza kama ilivyoweza kuthibitishwa na Waziri wa usalama.

 

Pia inaongeza kuwa kuwe na ulinzi wa kutosha katika makazi ya Rais mstaafu mijini na vijijini.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!