Home » ODM Yamtaka Naibu Gavana Wa Siaya Kujiuzulu

Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) kimemshauri Naibu Gavana wa Siaya William Oduol kujiuzulu na kumfungulia njia Gavana James Orengo kuteua naibu mpya.

 

Katibu wa ODM katika Masuala ya Kisiasa Opiyo Wandayi anasema hii ni kutokana na mifarakano kati ya viongozi hao wawili katika muda wa wiki chache zilizopita, ambayo iliishia kwa kutatiza kwa ghasia za mazishi waliyohudhuria hivi majuzi.

 

Katika kisa cha Mei 13, waombolezaji walilazimika kukimbia maziko ya aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Utumishi wa Umma Kaunti ya Siaya, Elijah Achoch, huku kukiwa na vitoa machozi na kupigwa risasi na polisi baada ya vijana washirika wa Orengo kumkatiza Oduol alipokuwa akiwahutubia waombolezaji.

 

Vikundi pinzani vilivurugana na askofu msimamizi alilazimika kukatisha mpango huo na kuwafungia nje viongozi wote.

 

Kupitia taarifa, Wandayi alisema kuwa mkwamo huo unaweza kutatiza utendakazi mzuri wa kaunti, na kuongeza kuwa utoaji wa huduma bora hauwezi kuhakikishwa “isipokuwa kitu kifanywe kuhusu uhusiano unaoonekana kuwa hatari” kati ya Orengo na Oduol.

 

Orengo na Oduol wamekuwa wakizozana kutokana na sababu kadhaa zikiwemo za ufisadi na tuhuma za kujiegemeza na mkwamo huo umesababisha ombi la wanaharakati watatu.

 

Alibainisha kuwa alikuwa amesoma ripoti ya Bunge la Kaunti ya Siaya kuhusu madai mbalimbali yaliyotolewa dhidi ya uongozi wa Orengo.
Akitaja wadhifa wa Oduol chini ya Gavana Orengo kuwa haukubaliki, Wandayi alimshauri Oduol kujiuluzu nafasi yake.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!