Home » ‘Nilishtuka!’ Shix Kapienga Asimulia Jinsi Alivyogongwa Na Gari

‘Nilishtuka!’ Shix Kapienga Asimulia Jinsi Alivyogongwa Na Gari

Muigizaji wa siku nyingi na mtangazaji wa redio, Shix Kapienga amezungumzia tukio lililotokea katika maisha yake na kumpa hofu na wasiwasi mkubwa ambao haujawahi kutokea tena katika maisha yake.

 

Kapienga anasema alipata ajali alipogongwa na gari alipokuwa akivuka barabara baada ya kutoka kutafuta chakula cha mchana huku akiharakisha kurejea studio.

 

Ni tukio ambalo lilitokea ghafla sana na kumuacha katika hali mbaya ya mshangao, jambo ambalo alisema hatalisahau katika maisha yake.

 

“Niligongwa na gari aina ya Nissan, gari lilinigonga nikiwa navuka barabara nikirudi studio ,nilivuka kununua baadhi ya sehemu na gari hii ilitokea ghafla na kunigonga. Nikiwa chini, gari lilipita juu ya mguu wangu. Nilishtuka, sijawahi kushtuka sana maishani mwangu,” Kapienga alisema.

 

Kapienga ambaye jina lake halisi ni Nancy Wanjiku Karanja alisema kuwa dereva wa gari hilo alishuka na kupigwa na butwaa alipoona hali yake, hadi ikabidi amuonee huruma licha ya kumgonga.

 

“Yule mzee dereva aliposhuka hata mimi nilimuonea huruma wakati anashuka hakuwa sawa, pia alikuwa kiwete mguu mmoja, nilijisikia vibaya lakini na wewe pia muda huo nilikuwa naumwa. ,” Kapienga alisema.

 

Shix ni mwigizaji, mcheshi na mshawishi ambaye pia amekuwa mtangazaji wa redio na TV.

 

Miongoni mwa miradi yake ya hivi punde zaidi ya filamu ni Baba Mapacha, filamu ya vichekesho inayopatikana kwenye Showmax.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!