Home » Gideon Moi Avunja Ukimya Juu Ya Maandamano Ya Azimio

Mwenyekiti wa Chama cha KANU Gideon Moi amezungumza kufuatia uharibifu wa mali ulioshuhudiwa siku za hivi majuzi huku upinzani ukiendelea kufanya maandamano dhidi ya serikali.

 

Tukio la hivi punde zaidi ni kuchomwa kwa kanisa na msikiti katika eneo la Kibra jijini Nairobi Jumatatu usiku, na wahuni baada ya siku ya maandamano.

 

Zaidi ya hayo, mali iliharibiwa wakati wahuni walipovamia kampuni ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga jijini Nairobi, pamoja na ardhi ya familia ya aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta katika Kaunti ya Kiambu, na Odinga ameishutumu serikali kwa kupanga uvamizi huo ili kukabiliana na maandamano yao.

 

Moi leo hii Jumatano, amesema ni lazima Wakenya wajizuie na uharibifu wa mali hata wanapotumia haki yao ya kikatiba ya kuandamana.
Kiongozi huyo amekashifu kuchomwa kwa kanisa la Kibra, ambapo Odinga ana wafuasi wengi.

 

Ingawa KANU iko chini ya chama cha muungano cha Azimio La Umoja One-Kenya ambacho Odinga anaongoza, chama hicho hakijashiriki maandamano ya Azimio huku upinzani ukishinikiza utawala wa Rais William Ruto kupunguza gharama ya maisha, miongoni mwa masuala mengine.

 

Jana Jumanne, chama hicho hata hivyo kilishutumu shambulio hilo kwenye shamba la Kenyatta, likilitaja kuwa la kuchukiza.

Kupitia kwa Katibu Mkuu wake George Wainaina, KANU iliitaka serikali kuhakikisha waliohusika na mashambulizi hayo wanatiwa mbaroni.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!