Home » Familia Meru Yatafuta Haki Ya Brenda Kawira 29

Familia moja ya Wameru inatafuta haki kwa jamaa yao mwenye umri wa miaka 29 anayedaiwa kuruka kutoka orofa ya nne ya nyumba aliyokuwa akiishi na mpenzi wake Kasarani.

 

Ilidaiwa kuwa Februari 21, 2023 Brenda Kawira aligombana na mpenzi wake na aliendelea kuruka futi 50 hadi kufa.

 

Shahidi pekee katika madai ya kujitoa uhai alikuwa mpenzi wake na ambaye alikiri kwamba waligombana.

 

Aidha Alidai kuwa Bi Kawira, akiwa amejawa na gadhabu, alitoka nje ya chumba cha kulala kilichoko orofa ya nne ya nyumba ya kupanga, akaenda kwenye balcony(pahala pa kutulia) na kuruka.

 

Mwanaume huyo aliwaambia polisi kwamba alisikia kelele na akaendelea kumtafuta katika vyumba vingine. Kisha akaenda kwenye balcony na baadaye kumwona chini.

 

“Nilienda kumtazama sebuleni, jikoni na vyumba vingine na hakuonekana. Kisha niliamua kwenda kwenye balcony na niliona mwili wake ukiwa umejawa na damu chini.”

 

Ripoti ya polisi kuhusu tukio hilo inaonyesha kuwa mpenzi huyo aliwataarifu majirani kadhaa ambao walimsaidia kumkimbiza katika hospitali kwenye barabara ya Thika ambako alitangazwa kuwa amefariki alipofika.

 

Uchunguzi wa kimwili uligundua majeraha yanayoonekana na michubuko usoni mwake. Ripoti ya uchunguzi wa maiti ilionyesha baadaye michubuko kwenye paja lake la kulia, upande wa kushoto wa shingo, shavu la kushoto na miguu.

 

Katika kifo chake, jamaa zake, marafiki na maafisa wa polisi waliozungumza na wanahabari wiki jana walieleza haja kubwa ya kutazama tena mfuatano wa matukio yaliyokatisha maisha ya Bi Kawira.

 

Kabla ya kifo chake, Alikuwa ameshinda udhamini wa kusomea Shahada ya Uzamili nchini Australia na angeondoka nchini Juni 2023.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!