Home » Mvulana Wa Miaka 6 Aliyempiga Risasi Mwalimu Hatashtakiwa

Mvulana mwenye umri wa miaka sita aliyempiga risasi mwalimu wake katika shule ya msingi katika jimbo la Virginia nchini Marekani huenda asishtakiwe, mwendesha mashtaka amesema.

 

Lakini mamlaka katika jiji la Newport News bado hawajaamua iwapo mtu mzima yeyote atakabiliwa na mashtaka ya jinai katika kesi hiyo.

Polisi wamesema mtoto huyo alibeba bunduki kwenye mkoba wake katika Shule ya Msingi ya Richneck tarehe 6 Januari.
Abigail Zwerner, mwalimu mwenye umri wa miaka 25, alipigwa risasi mkononi na kifuani, lakini akanusurika.
Siku ya jana Jumatano, Wakili wa Jumuiya ya Madola ya Newport News, Howard Gwynn aliambia NBC kwamba ofisi yake haitatafuta mashtaka dhidi ya mvulana huyo.

 

Alisema “matarajio kwamba mtoto wa miaka sita anaweza kushtakiwa ni shida” kwa sababu mtoto ni mdogo sana kuelewa mfumo wa sheria.

 

“Lengo letu si tu kufanya jambo haraka iwezekanavyo,” . Gwynn aliongeza.
“Pindi tutakapochambua ukweli wote, tutamfungulia mashtaka mtu yeyote au watu ambao tunaamini tunaweza kuthibitisha bila shaka kuwa walitenda uhalifu.”

 

Katika mahojiano tofauti na chombo cha habari nchini humo,. Gwynn alisema kwamba makubaliano ya jumla kati ya wataalam wa sheria wa Marekani ni kwamba mtoto wa miaka sita “hawezi kuunda dhamira ya uhalifu inayohitajika kuwa na hatia ya shambulio kali”.

 

Bi. Zwerner anashtaki wilaya ya shule baada ya kupigwa risasi mkononi na sehemu ya juu ya kifua kufuatia kile polisi walichoeleza kuwa “kugombana” na mwanafunzi wa darasa.

 

Silaha hiyo ilinunuliwa kihalali na ilikuwa ya mama wa mtoto huyo, polisi wamesema.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!