Home » Gachagua Amkashifu Raila

Naibu Rais Rigathi Gachagua amemsuta kiongozi wa Azimio La Umoja One Kenya Coalition Party Raila Odinga kuhusu upinzani wake wa mara kwa mara dhidi ya Mswada wa Fedha wa 2023 ambao miongoni mwa mambo mengine unapendekeza kuanzishwa kwa hazina ya nyumba za bei nafuu.

 

DP Gachagua ambaye alizungumza mjini Nyeri Alhamisi amesisitiza kuwa Mswada huo ni mzuri kwa nchi, akidai kuwa Wakenya wote wenye nia njema wanaunga mkono mswada huo kando na kiongozi wa Upinzani.

 

Huku akirejelea kuwa Odinga amekuwa akipinga pendekezo lolote ‘nzuri’ kwa taifa, DP alimkemea chifu huyo wa Azimio akidai kuwa waziri mkuu huyo wa zamani anawapotosha Wakenya.

 

Gachagua wakati uo huo amedai kuwa eneo la Mlima Kenya ndilo lililounga mkono kikamilifu mswada huo tata na kwamba wabunge wote washirika wa Kenya Kwanza watahakikisha mswada huo umepitishwa bungeni.

 

Matamshi ya DP yalikuja kama rejea kwa Odinga ambaye amedumisha upinzani wake kwa mswada huo na kuutaja kuwa hujuma ya kiuchumi ambayo itaathiri walipa kodi.

 

Kiongozi huyo wa upinzani anashikilia kuwa mswada huo unapaswa kuondolewa kwa kushindwa kuongoza maandamano ya nchi nzima.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!